#Football #Sports

TUSKER WAWANIA USHINDI WA KWANZA KAGAME CUP

Tusker wanatarajia kurejea katika njia ya ushindi watakapovaana na wenyeji Rayon Sports katika mchezo wa Kundi C wa mashindano ya CECAFA Kagame Cup utakaochezwa jijini Kigali, Rwanda

Mabingwa hao wa Kombe la Mozzartbet  wanatafuta alama zao za kwanza baada ya kupoteza mabao 2-0 dhidi ya Al Hilal katika mchezo wao wa ufunguzi wa mashindano hayo

Rayon Sports wanaingia katika pambano hilo wakiwa na morali ya juu baada ya kuanza kampeni yao kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya KVZ FC, matokeo yaliyowaweka kileleni mwa kundi kwa alama tatu pamoja na Al Hilal.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *