SONKO AONYA UPINZANI DHIDI YA MGAWANYIKO
Wakati viongozi wa upinzani wakizidi kuonyesha nia ya kuwania urais mwaka 2027, hofu inaongezeka kwamba mgawanyiko unaweza kudhoofisha uwezo wao wa kushindana dhidi ya Rais William Ruto.
Aliyekuwa Gavana wa Nairobi Mike Sonko ameonya viongozi wa upinzani kuwa wanapaswa kuungana nyuma ya mgombea mmoja wa urais ili kuongeza nafasi ya kushinda uchaguzi mkuu.
Sonko amesema kuwasimamisha wagombea wengi kutagawanya kura za upinzani na kumpa Rais William Ruto nafasi kubwa ya kutetea kiti chake kwa muhula wa pili.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 














































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































