#Local News

IEBC YAENDESHA USHIRIKISHWAJI WA UMMA KUHUSU UFADHILI WA KAMPENI

Maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2027 yanaendelea kushika kasi, huku juhudi zikiongezwa kuhakikisha mchakato wa uchaguzi unakuwa wa haki, uwazi na unaoaminika kwa wananchi wote.

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) inaendesha vikao vya ushirikishwaji wa umma kote nchini ili kukusanya maoni kuhusu kanuni zinazopendekezwa za ufadhili wa kampeni za kisiasa.

IEBC imesema kanuni hizo zinalenga kuimarisha uwazi na usawa katika kampeni za kisiasa, huku ikiwahakikishia Wakenya kuwa iko tayari kusimamia uchaguzi wa mwaka 2027 kwa njia huru, ya haki na yenye kuaminika.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *