#Local News

INGONGA AONYA WANASIASA WANAOCHOCHEA GHASIA

Kauli za kisiasa zinazoweza kuchochea chuki na vurugu zimeanza kuvutia uangalizi mkali wa vyombo vya sheria huku joto la siasa za uchaguzi mkuu wa mwaka 2027 likizidi kupanda.

Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma Renson Ingonga ameonya wanasiasa na watu binafsi kuwa hakuna atakayeachwa iwapo atapatikana akichochea chuki, ghasia au kuhatarisha amani ya nchi.

Ingonga amesema wahusika watakabiliwa na mkono wa sheria huku akiwataka viongozi na wafuasi wao kudumisha amani na kujiepusha na vitendo vinavyoweza kuvuruga utulivu wa taifa.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *