MGOMO WA WAUGUZI WAZIDI KUVURUGA HUDUMA ZA AFYA
Tumaini la maelfu ya wagonjwa kupata matibabu katika hospitali za umma linaendelea kufifia, huku mgomo wa wauguzi na wakunga ukizidi kuathiri utoaji wa huduma za afya katika kaunti mbalimbali.
Wauguzi na wakunga wanaendelea na mgomo ulioingia siku ya pili, hali iliyosababisha huduma za afya kusimama katika hospitali nyingi za umma nchini.
Wagonjwa walikosa matibabu katika kaunti za Kericho, Kisumu, Machakos, Embu, Tharaka Nithi na maeneo mengine baada ya hospitali nyingi kushindwa kutoa huduma kutokana na mgomo huo.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 



























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































