GAVANA WA MOMBASA AMEAGIZA KUAJIRIWA KWA WAHUDUMU WAPYA WA AFYA
Gavana wa Mombasa, Abdulswamad Nassir, ameagiza kuajiriwa kwa wahudumu wapya wa afya ili kuongeza idadi ya wafanyakazi katika vituo vya matibabu vya kaunti hiyo.
Gavana Nassir amesema hatua hiyo inalenga kuboresha utoaji wa huduma za afya na kupunguza changamoto ya upungufu wa wahudumu katika hospitali na vituo vya afya.
Hatua hiyo imechukuliwa wakati sekta ya afya ikikabiliwa na changamoto mbalimbali, huku serikali za kaunti zikiendelea kutafuta njia za kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za matibabu.
Imetayarishwa na Jesca Angeyo
English 



























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































