#Local News

SENETA DAN MAANZO ASEMA HAKUNA UWEZEKANO WA KALONZO KUJIUNGA NA SERIKALI YA KENYA KWANZA

Seneta wa Makueni Dan Maanzo amesema hakuna uwezekano wa kiongozi wa Chama cha Wiper Democratic Movement, Kalonzo Musyoka, kujiunga na serikali ya Kenya Kwanza kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2027.

Maanzo ambaye ni mshirika wa karibu wa Kalonzo amesema hakuna mazungumzo yanayoendelea kati ya Kalonzo na Rais William Ruto kuhusu ushirikiano wa kisiasa.

Kauli ya Maanzo inajiri huku mijadala ya kisiasa ikiendelea kuhusu miungano ya vyama mbalimbali vinavyojiandaa kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2027.

Imetayarishwa na Jesca Angeyo

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *