#Football #Sports

BEN WHITE AITWA TIMU YA UINGEREZA

Mlinzi wa Arsenal, Ben White, ametajwa katika kikosi cha uingereza kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya miaka mitatu.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 hajahusiana na timu tangu alipoondoka kambi ya Kombe la Dunia 2022 Qatar kwa sababu binafsi, na baadaye kujitokeza kuwa hafai kuchaguliwa chini ya kocha Gareth Southgate.

Uingereza itacheza mechi za kirafiki dhidi ya Uruguay tarehe 27 Machi na Japan tarehe 31 Machi katika Uwanja wa Wembley, huku White akichukua nafasi ya Jarell Quansah aliyepoteza nafasi kutokana na jeraha la mguu.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *