MSIHOFU KUHUSU MAFUTA, SERIKALI
Serikali imewahakikishia wakenya kwamba kuna hifadhi ya kutosha ya mafuta nchini licha ya kufungwa kwa eneo la bahari la usafirishaji wa mafuta la Hormuz katika eneo la Mashariki ya Kati, ikisema taifa lina akiba ya kutosha ya mafuta.
Kwa mujibu wa Waziri wa kawi Opiyo Wandayi, wananchi hawana sababu ya kuwa na wasiwasi na kwamba mfumo wa usambazaji wa mafuta uko imara.
Amezionya kampuni za mafuta dhidi ya kuficha bidhaa hiyo kwa lengo la kuuza kwa bei ghali baadaye.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 
































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































