IEBC YAWAHIMIZA VIJANA KUSAJILIWA
Tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC imesema inalenga kuwasajili wapiga kura wapya milioni 6.5 kabla ya uchaguzi mkuu ujao, tume hiyo ikihimiza ushirikiano miongoni mwa washikadau ili kuafikia lengo hilo.
Kwa mujibu wa mwenyekiti wa tume hiyo Erastus Ethekon, awamu ya kwanza ya zoezi la kitaifa lililoanza katika wadi zote hapo jana, inatarajiwa kukamilika tarehe 28 mwezi ujao.
Vijana wameendelea kuhimizana kujisajili kwa wingi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 
































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































