#Local News

MAANDAMANO KENYA YAONGEZEKA KWA ASILIMIA 29

Kenya ilishuhudia maandamano 453 katika kipindi cha miezi sita ya kwanza ya mwaka 2026, ikiwa ni ongezeko la asilimia 29 ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2025.

Kwa mujibu wa shirika la Amnesty International, ongezeko hilo limechangiwa zaidi na kupanda kwa gharama ya maisha, bei ya mafuta na malalamiko kuhusu hali ya uchumi.

Ripoti hiyo imeonyesha kuwa jumla ya maandamano 1,292 yalirekodiwa nchini kati ya Januari 2025 na Juni 2026, huku mwaka 2025 ukishuhudia maandamano 839.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *