#Football #Sports

MOH SALAH AJIUNGA NA TRABZONSPOR

Mohamed Salah amekamilisha uhamisho wake kwenda Klabu ya Trabzonspor baada ya klabu hiyo kuthibitisha kufikiwa kwa makubaliano ya kumsajili mshambuliaji huyo wa Misri.

Salah amejiunga na Trabzonspor kwa mkataba wa miaka miwili kama mchezaji huru, baada ya kuondoka katika Liverpool baada ya kumalizika kwa mkataba wake na klabu hiyo.

Uhamisho huo unafungua ukurasa mpya katika maisha ya soka ya nyota huyo, anayetarajiwa kuiongoza Trabzonspor katika kusaka ubingwa wa ligi nchini uturuki.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

MOH SALAH AJIUNGA NA TRABZONSPOR

GOR MAHIA YATINGA FAINALI CECAFA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *