#Local News

RUTO AMSUTA UHURU, ASEMA ANAPANGA KUMNG’OA MADARAKANI

Rais William Ruto amemkosoa tena mtangulizi wake, akimtuhumu kufadhili upinzani katika juhudi za kudhoofisha serikali yake na kumng’oa mamlakani.

Akizungumza na wakazi wa Eldoret, Kaunti ya Uasin Gishu, Ruto amesema serikali ya iliyopita haikushughulikia ipasavyo masuala kama makazi ya bei nafuu na huduma ya afya kwa wote wakati wa utawala wake.

Ruto amesema serikali yake inapaswa kuhukumiwa kwa rekodi ya utendakazi, akiwakosoa wapinzani kwa kutumia kauli za kisiasa kama “wantam” na “must go” bila kuwasilisha mpango mbadala wa kuwaongoza Wakenya.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *