#Rugby #Sports

CHIPU YATAWALA AFRIKA BAADA YA USHINDI WA BARTHES TROPHY

Timu ya Kenya ya raga ya vijana chini ya miaka 20, Chipu, imeibuka mabingwa wa Afrika baada ya kuifunga Namibia kwa alama 33-14 katika fainali ya Barthés Trophy nchini Uganda.

Chipu ilifika fainali baada ya kuishinda Zimbabwe 35-21 katika nusu fainali, na kukamilisha kampeni yake kwa ushindi uliothibitisha ubora wa Kenya katika raga ya vijana barani Afrika.

Nahodha wa Simbas, Samuel Asati, amepongeza kikosi hicho kwa kiwango chake, akisema ushindi huo ni ishara ya nguvu na mustakabali mzuri wa raga ya Kenya.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *