MAHAKAMA YASITISHA UTUMIZI WA VYETI VYA KIDIJITALI VYA USAJILI WA MAGARI
Mahakama Kuu imeiagiza Mamlaka ya Kitaifa ya Uchukuzi na Usalama Barabarani NTSA kuendelea kutambua vyeti vya usajili wa magari vya karatasi huku ikisubiri kusikilizwa na kuamuliwa kwa kesi inayopinga kuanzishwa kwa vyeti vya kidijitali.
Jaji Patricia Nyaundi Mande ametoa amri hiyo ya muda katika kesi iliyowasilishwa na Javan Onyango na Emmanuel Kiplagat, ambao wamepinga utekelezaji wa mfumo mpya wa kidijitali wa usajili wa umiliki wa magari unaosimamiwa na NTSA.
Imetayarishwa na Hilda Ajema
English 



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































