#Local News

RUTO KUKUTANA NA WAKENYA 5,000 KUJADILI RUWAZA 2060

Rais William Ruto leo anatarajiwa kukutana na zaidi ya Wakenya 5,000 kutoka kaunti zote 47 katika ukumbi KICC kwa mazungumzo ya kitaifa kuhusu mpango wa Ruwaza ya Kenya 2060.

Mazungumzo hayo yataashiria kuanza rasmi kwa ushirikishwaji wa umma huku wananchi wakitarajiwa kutoa maoni kuhusu vipaumbele vya maendeleo ya muda mrefu.

Mapendekezo yatakayowasilishwa na washiriki hao yanatarajiwa kuwa msingi wa Mkataba wa Kitaifa wa Maendeleo, ambao baadaye utabadilishwa kuwa Mswada na kuwasilishwa Bungeni kwa ajili ya kuzingatiwa.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *