#Local News

ODM YAMSUTA GACHAGUA KWA KAULI KUHUSU KIFO CHA RAILA

Chama cha ODM kimemkosoa vikali kiongozi wa DCP Rigathi Gachagua kuhusu kauli zake zinazotia shaka mazingira ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu na mwanzilishi wa chama hicho, Raila Odinga.

Mwenyekiti wa ODM Gladys Wanga amesema madai ya Gachagua kuhusu uwezekano wa mchezo mchafu katika kifo cha Raila hayana msingi na yanaweza kuongeza mgawanyiko nchini, wakati familia yake bado inaomboleza.

Wanga pia amekanusha uwezekano wa ODM kushirikiana na Gachagua, akimtuhumu kiongozi huyo wa DCP kuendeleza siasa za kikabila na zinazogawanya Wakenya.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *