MAUAJI YA WAKILI YAIBUA MASWALI
Polisi jijini Nairobi wanachunguza mauaji ya kikatili ya wakili Kyalo Mbobu, aliyepigwa risasi na kuuawa papo hapo kwenye barabara ya Langa’ata na mtu aliyekuwa akitumia pikikipiki usiku wa kuamkia leo.
Walioshuhudia wanasema wakili huyo alikuwa pekee yake kwenye gari hilo, mauaji hayo yakikosolewa na chama cha wanasheria nchini LSK ambayo imeyataja kuwa tishio kwa utendakazi wa mawakili.
Mbobu mwenye tajriba ya zaidi ya miaka 29 kama wakili, aliwahi kuhudumu kama naibu mwenyekiti wa jopokazi la kutatua mizozo ya vyama vya kisiasa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































