#Local News

AMISI ADAI RUTO ALINUNUA ODM

Mbunge wa Saboti kaunti ya Trans Nzoia, Caleb Amisi, amehusisha masaibu ya chama cha ODM na mwingilio kutoka nje ya chama, akiibua madai kwamba Rais William Ruto amekinunua chama hicho huku wanachama chipukizi wakikabiliwa na vitisho vya kufurushwa.

Akizungumza wakati wa zoezi la kuwapokeza wanafunzi hundi za basari katika eneo la Matisi, Amisi amesema waliolengwa ni pamoja na mwanawe kinara mwanzilishi wa chama hicho Raila Odinga, Winnie Odinga, seneta Edwin Sifuna na mbunge Babu Owino.

Amekariri kuwa viongozi hao hawatayumbishwa.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

AMISI ADAI RUTO ALINUNUA ODM

RUTO: MSIWAPOTOSHE VIJANA

AMISI ADAI RUTO ALINUNUA ODM

MGAWANYIKO ODM: KINARA ALAUMIWA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *