#Local News

VIONGOZI WA KENYA KWANZA KIPSIGIS WAMKOSOA GACHAGUA

Viongozi wa muungano wa Kenya Kwanza kutoka jamii ya Kipsigis wamemkashifu aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua kwa matamshi yake kuwa jamii ya Kalenjin haina kiongozi anayezungumza kwa niaba yake.

Viongozi hao wakiongozwa na Kiongozi wa Wengi katika bunge Seneti, Aaron Cheruiyot, wamesema kauli za Gachagua hazina msingi na zinalenga kuleta ubabe wa kisiasa ndani ya jamii hiyo.

Aidha wamesema jamii ya Kalenjin ina viongozi wake halali na kwamba si sahihi kwa mtu yeyote kudai kuwa hakuna uongozi unaowakilisha maslahi yao.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

VIONGOZI WA KENYA KWANZA KIPSIGIS WAMKOSOA GACHAGUA

MBUNGE MANYATTA AMKOSOA WAZIRI WA USALAMA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *