#Local News

ICHUNG’WAH NA NYORO WAZOZANA BUNGENI BAADA YA KUONDOKA UDA

Kiongozi wa Wengi katika Bunge la Kitaifa Kimani Ichung’wah na Mbunge wa Kiharu Ndindi Nyoro wamezozana vikali Bungeni kufuatia uamuzi wa Nyoro kuondoka katika chama tawala cha UDA.

Mzozo huo umeibua madai ya upendeleo katika mgao wa bajeti huku Nyoro akitangaza kujiunga na People’s Party of Kenya na kuikosoa serikali kwa kushindwa kutimiza ahadi zake.

Nyoro pia ameishutumu serikali kwa madai ya kufadhili makundi ya vijana kuvuruga Wakenya, huku mzozo huo ukiongeza dalili za mgawanyiko wa kisiasa ndani ya muungano unaoongoza serikali.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *