OWALO: KENYA BADO HAIJAKOMAA KISIASA BAADA YA MIAKA 30
Aliyekuwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Uchumi wa Kidijitali Eliud Owalo amesema inasikitisha kuwa zaidi ya miongo mitatu tangu Kenya kuingia katika mfumo wa vyama vingi, baadhi ya watu bado hawajaelewa umuhimu wa ushindani mzuri wa kisiasa.
Owalo amesema ushindani wa kisiasa unapaswa kuwa sehemu ya demokrasia na si sababu ya kuleta uhasama, chuki au migawanyiko miongoni mwa wananchi.
Ametaka viongozi na wafuasi wa vyama mbalimbali kuheshimu misimamo tofauti ya kisiasa na kuruhusu ushindani wa haki na wa amani katika kuelekea uchaguzi mkuu wa 2027.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 


































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































