WAMALWA: GHASIA ZINAWEZA KUIREJESHA KENYA ICC
Kiongozi wa chama cha DAP-K Eugene Wamalwa ameonya kuwa Kenya inaweza kujikuta tena mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu ICC iwapo ghasia za kisiasa zitaendelea kushika kasi.
Wamalwa amesema hali inayoshuhudiwa sasa inalikumbusha taifa machungu ya ghasia za uchaguzi wa 2007 na 2008, akisisitiza kuwa siasa za vurugu zinaweza kuwa na madhara makubwa kwa nchi na viongozi wanaohusika.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 


































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































