#Football #Sports

TOTTENHAM YAFIKIA MAKUBALIANO YA KUMSAJILI SAVINHO

Tottenham imefikia makubaliano ya awali na Manchester City kumsajili mshambuliaji Savinho, huku ada ya uhamisho ikitarajiwa kuzidi pauni milioni 75.

Savinho anatarajiwa kusafiri kwa ajili ya vipimo vya afya kabla ya kukamilisha uhamisho wake, huku maelezo ya mwisho kuhusu ada hiyo yakisubiriwa.

Tottenham pia ina matumaini ya kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa Misri Omar Marmoush, huku mazungumzo yakiwa katika hatua za juu na masharti binafsi ya mchezaji huyo tayari yakiwa yamekubaliwa.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *