#Local News

UCHUNGU WA SUKARI WAENDELEA KUJITOKEZA

Wabunge kutoka Magharibi mwa nchi wametishia kuelekea mahakamani ili kushinikiza kubatilishwa kwa mchakato wa kukodishwa kwa kiwanda cha miwa cha Nzoia, wakidai serikali imekiuka sheria katika kumkabidhi mwekezaji wa kibinafsi usimamizi wa kiwanda hicho.

Wakizungumza na wanahabari jijini Nairobi, viongozi hao wameishutumu serikali kwa wanachosema kukosa uwazi katika mchakato huo.

Miongoni mwao ni seneta wa Vihiga Godfrey Otsotsi, Edwin Sifuna wa Nairobi na mwenzake wa Busia Okiya Omtatah na mbunge wa Kabuchai Majimbo Kalasinga.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *