KENYA YAZUNGUMZIA KUFURUSHWA KWA KARUA
Serikali imetangaza kuwachukulia hatua kali za kisheria viongozi na wakenya kwa jumla wanatoa kauli za uchochezi, ikisema matamshi ya baadhi ya viongozi yanafufua makovu ya ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007.
Katika kikao na wanahabari jijini Nairobi, msemaji wa serikali Isaac Mwaura amewakosoa viongozi hao ambao hakuwataja, akisisitiza serikali itafanya kila iwezalo kuwahakikishia wananchi utulivu.
Aidha, Mwaura ametetea hatua ya serikali ya Tanzania kumfurusha kinara wa chama cha PLP Martha Karua kutoka nchini humo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































