SERIKALI YAAPA KUMWAJIBISHA GACHAGUA
Serikali imewatahadharisha wakenya dhidi ya kuhudhuria mikusanyiko ya kumkaribisha nyumbani kinara wa chama cha DCP Rigathi Gachagua atakaporejea nchini hii leo kutoka Marekani iwapo mikusanyiko hiyo hatitakuwa na kibali.
Katika kikao na wanahabari, waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen na inspekta mkuu wa polisi Douglas Kanja, wamesema serikali haitaruhusu vikao vya kutatiza amani na biashara kufanyika nchini.
Gachagua anayerejea leo baada ya ziara ya wiki 6, ameratibiwa kufanya mkutano wa hadhara katika uwanja wa Kamukunji mtaani Shauri Moyo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































