#Local News

NCA YADAI JENGO HALIKUWA LIMESAJILIWA

Imebainika kwamba jengo lililoporomoka mtaani Karen jijini Nairobi Jumamosi iliyopita halikuwa limesajiliwa inavyohitajika kisheria.

Haya ni kulingana na mamlaka ya kitaifa inayosimamia mijengo NCA, ikisema kuwa uchunguzi wa awali umeashiria dosari katika muundo wa jengo hilo la ghorofa moja lililoporomoka kutokana na uzito wa zege.

Watu wawili walifariki, wawili wakapata majeraha mabaya huku wengine 7 wakitibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

NCA YADAI JENGO HALIKUWA LIMESAJILIWA

MASAIBU YA UNITED YAZIDI KIWANGO

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *