HOFU YAWAKUMBA WAFANYABIASHARA KUHUSU WIZI WA KUTISHA
Wafanyabiashara katikati mwa jiji la Nairobi wameingiwa na hofu ya kiusalama baada ya genge la majambazi kuvunja duka moja la vifaa vya kielektroniki na kutoweka na bidhaa zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 16.
Kamera za CCTV eneo hilo ziliwanasa washukiwa wakizungumza na walinzi ila baadaye walinzi wanaonekana kupoteza fahamu kabla ya wizi huo kutekelezwa, mmiliki wa duka hilo Moses Mwangi akisema nyingi ya bidhaa zilikuwa za mkopo.
Polisi kutoka kituo cha Central wameanzisha uchunguzi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































