KAUNTI YA NAIROBI YAORODHESHA MALI KWA MNADA
Serikali ya kaunti ya Nairobi imetishia kuvipiga mnada vipande vya ardhi katikati ya jiji kwa madai ya kukosa kulipia ada za arthi nchini.
Katika notisi ya kurasa 72 iliyochapishwa leo Ijumaa, Gavana Johnson Sakaja ameonya kuwa kushindwa kulipa viwango vya ardhi kutasababisha kupigwa mnada kwa sehemu husika za ardhi.
Sehemu ya arthi iliyoorotheshwea katika notisi hiyo inapatikana katika maeneo bunge ya Westlands , Starehe, Ruaraka, Roysambu Mathare, Makandara Langata, Kasarani Kibra Embakasi Magharibi , Embakasi mashariki, Dagoreti kusini na Dagoreti kaskazini.
Imetayarishwa na: Janice Marete
English 















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































