MAAFISA 11 WA KAUNTI YA VIHIGA WAKAMATWA KWA WIZI WA MILIONI 17
Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi imewakamata maafisa 11 katika Serikali ya Kaunti ya Vihiga huku ikianzisha uchunguzi kuhusu tuhuma za wizi wa Shilingi milioni 17 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha kuongeza damu.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari tume hiyo waliokamatwa ni pamoja na Afisa Mkuu wa Huduma za Matibabu Dkt Arnold Kimiyia Mamadi na Mkurugenzi wa Ununuzi Godfrey Oyaro.
Ni miongoni mwa washukiwa 11 wanaotarajiwa kufikishwa mbele ya Mahakama ya Kupambana na Ufisadi ya Kakamega hii leo.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































