SI VIKAO VYA TIKTOK, KINGI AONYA MASENETA
Huku vikao vya kusikiliza hoja ya kumtimua kutoka mamlakani naibu rais Rigathi Gachagua vikiendelea kwa siku ya pili na mabayo inatarajiwa kuwa ya mwisho hii leo, spika wa bunge la senati Amason Kingi amewataka maseneta kuchukulia vikao hivyo kwa uzito.
Akitoa onyo ya kuwatimua baadhi ya maseneta, Spika Kingi amesema hoja hiyo ni suala zito kwa taifa na hivyo kanuni za seneti zinapaswa kuzingatiwa kwenye mchakato huo.
Onyo ya Spika Kingi imejiri kufuatia minong’ono kutoka kwa maseneta baada yao kupewa fursa ya kuwauliza mashahidi maswali kutoka tume ya EACC.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 
























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































