#Local News

MALALAH ATAKA VIONGOZI WA UPINZANI WAAPE KUTOKUSALITI UMOJA

Naibu Kiongozi wa DCP Cleophas Malalah amewataka viongozi wote wanaolenga kuunda muungano wa upinzani kuweka ahadi ya wazi kwamba watabaki pamoja hadi mwisho wa safari.

Malalah amesema kila kiongozi anapaswa kutia saini ahadi binafsi ya kuendeleza umoja huo, hata iwapo hatateuliwa kuwa mgombea wa urais wa muungano, akisema hatua hiyo itajenga uaminifu miongoni mwa washirika.

Amesisitiza  kuwa lengo kuu linapaswa kuwa ushindi wa upinzani katika uchaguzi wa 2027.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *