UJENZI WA AFUENI WEBUYE
Huduma za matibabu katika kaunti ya Bungoma zinatarajiwa kuimarika kutokana na ujenzi unaoendelea wa jumba la ghorofa mbili katika hospitali ya rufaa ya kaunti ndogo ya Webuye itakayosaidia kupunguza msongamano wa wagonjwa unaoshuhudiwa kwa sasa eneo hilo.
Akizungumza baada ya kukagua ujenzi huo, gavana wa kaunti ya Bungoma Ken Lusaka amekiri kuwepo kwa changamoto za msongamano wa wagonjwa, akidokeza kuwa kuna mikakati ya kupandisha cheo hospitali hiyo na ile ya Bungoma.
Kwa upande wake msimimizi wa hospitali hiyo David Wanikina, amekariri afueni itakayoletwa na mradi huo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































