#Football #Sports

AYANY ATAKA NAIVAS KULIPIZA KISASI DHIDI YA LUANDA VILLA

Kocha mkuu wa Naivas FC, Elvis Ayany, amesema timu yake imejipanga kulipiza kisasi watakapokutana na Luanda Villa mwishoni mwa wiki katika mechi ya ushindani mkali ya Ligi ya Daraja la Kwanza.

Ayany amesema kumbukumbu ya kichapo cha bao 1-0 walichopata katika mechi ya awali imewapa motisha ya kubadili matokeo safari hii.

Hata hivyo, kocha huyo amewaonya wachezaji wake dhidi ya kubeza wapinzani wao licha ya changamoto za hivi karibuni za Luanda Villa, akisisitiza umuhimu wa kuwa makini na kudumisha umakini kwa muda wote wa mchezo.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

AYANY ATAKA NAIVAS KULIPIZA KISASI DHIDI YA LUANDA VILLA

KANYI AIAMINI HARAMBEE STARLETS WAFCON

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *