TUTAWATIBU MKIUMIA KATIKA MAANDAMANO; USHIRIKA WA MATIBABU
Huku maandamano ya Occupy Bunge yakiingia siku ya pili, Muungano wa Madaktari, Wafamasia na Madaktari wa Meno nchini Kenya (KMPDU) umetangaza kushiriki kwa wanachama wake, kwa mpango wa kutoa huduma za matibabu kwa waandamanaji.
Katibu Mkuu wa KMPDU Davji Atellah amesema madaktari watashughulikia watakaopata majeraha kwa dharura ambazo zinaweza kutokea kutokana na maandamano yaliyopangwa katika miji yote ya Kenya.
Madaktari hao wananuia kukusanyika Nairobi na miji mingine mchana kuungana na waandamanaji wengine.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 



























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































