BUNGE KUANZA KIKAO MAPEMA
Bunge la Kitaifa litarejea kwa kikao chake cha mwisho mapema kuliko ilivyo kawaida ili kuwapa wabunge muda wa kutosha kufanya kampeni kabla ya Uchaguzi Mkuu ujao.
Kulingana na Karani wa Bunge la Kitaifa, Samuel Njoroge, kikao hicho ambacho kwa kawaida huanza mwezi Februari sasa kitaanza mapema mwezi Januari mwaka ujao katika mwaka wa mwisho wa muhula wa Bunge.
Njoroge amesema hatua hiyo inalenga kuhakikisha wabunge hawapati hasara ya kisiasa kwa kusalia Nairobi ilhali wapinzani wao wako mashinani wakihamasisha wapiga kura.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 





































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































