PATRICK ODHIAMBO ATUA KCB
Klabu ya soka ya KCB imemteua aliyekuwa kocha mkuu wa Kakamega Homeboyz Patrick Odhiambo kuwa kocha mkuu mpya.
Odhiambo anachukua nafasi ya mshambuliaji wa zamani wa Hararambee Stars Bernard Mwalala kwa kandarasi ya mwaka mmoja, na anatarajiwa kuinoa KCB hadi Julai 16, 2025.
Odhiambo alishinda taji la KPL kama msaidizi wa Steven Pollack huko Gor Mahia 2019/2020.
Wanabenki hao waliachana na Mwalala baada ya kuamua kuchukua mapumziko ili kutafuta Leseni yake ya Caf A ya ukocha, hitaji la Shirikisho la Soka la Kenya katika kanuni mpya za makocha wakuu wote wa KPL.
Imetayarishwa na Nelson Andati
English 





































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































