‘KATIBU MKUU BANDIA’ UDA AJERUHIWA
Joe Khalende aliyejitangaza kuwa katibu mkuu wa chama tawala cha UDA sasa anauguza majeraha baada ya kusambuliwa na watu wanachama wanaoaminika kuwa wafuasi wa katibu mkuu Cleophas Malala katika makao makuu ya chama hicho.
Khelende amepata majeraha kichwani, akidai kwamba kuna watu walio na njama ya kummwangamiza.
Kundi la watu waliomshambulia limekuwa likiimba nyimbo za kumsifia Malala.
Awali, mwenyekiti wa UDA Cecil Mbarire, alipinga madai ya kwamba Khalende ndiye katibu mkuu mpya wa chama hicho.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































