MSHUKIWA MKUU WA WIZI WA MTIHANI WA KCSE AKAMATWA HUKO NAKURU
Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI) imemkamata mwanamume anayedaiwa kuwa mmoja wa wahalifu wanaotafutwa sana nchini Kenya kwa kuhusika na udanganyifu wa mtihani wa KCSE wa 2024 na anatarajiwa kufikishwa mahakamani hii leo.
Kulingana na dci Collins Kipchumba Kemboi mwenye umri wa miaka 23 anashirikiana na Dorothy Jerop Kiprono kuendesha mifumo ya uvujaji wa mitihani kwenye mitandao yaTelegram na WhatsApp,
Inadaiwa ana wafuasi zaidi ya 78,000 kwenye Telegram na zaidi ya 8,500 katika vikundi vyake vya WhatsApp.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































