WAKULIMA TRANS NZOIA WATAKA BEI YA MBOLEA KUFIKA SHILINGI 1,500
Wakulima katika Kaunti ya Trans Nzoia wamekaribisha hatua ya serikali kupunguza bei ya mbolea, wakisema itawapunguzia gharama za uzalishaji.
Hata hivyo, wakulima hao wameitaka serikali kufanya punguzo zaidi ili bei ya mfuko wa mbolea ishuke hadi shilingi 1,500.
Wamesema bei nafuu ya mbolea itawasaidia kupunguza gharama za kilimo na kuongeza uzalishaji wa chakula, huku wakiitaka serikali kuendelea kuweka mikakati ya kuwasaidia wakulima kukabiliana na gharama za uzalishaji.
Imetayarishwa na Hilda Ajema
English 


















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































