#Local News

OGAMBA AONYA DHIDI YA SIASA SHULENI

Waziri wa Elimu Julius Ogamba amewaonya viongozi wa kisiasa dhidi ya kuingiza siasa katika masuala ya elimu, akisema hulka hizo zinaibua hofu miongoni mwa wazazi na wanafunzi nchini.

Akizungumza katika kaunti ya Murang’a, Ogamba amerejelea kauli ya aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua kwamba wanafunzi wajiunge na shule za kitaifa zilizo katika maeneo wanakotoka, akisisitiza kuwa lengo la shule za kitaifa ni kuwahudumia wanafunzi kutoka maeneo yote ya taifa.

Amekariri haja ya shule hizo kutoa nafasi sawa kwa wanafunzi.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

OGAMBA AONYA DHIDI YA SIASA SHULENI

ODM YAANDAA NDOA NA UDA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *