KENYA KUPOKEA UFADHILI WA MIUNDOMBINU
Miundombinu ya kidijitali nchini inatarajiwa kuimarika kutokana na ufadhili wa shilingi bilioni 50 kutoka kwa benki ya dunia, ambao Kenya imeratibiwa kupokea katika kipindi cha miaka 3 ijayo kuboresha miundombinu hiyo.
Fedha hizo zitatumika kwenye upanuzi wa kasi ya huduma za intaneti, lengo likiwa ni kuwavutia wawekezaji wapya katika sekta ya teknolojia.
Tim Kelly ni mtaalam mkuu wa masuala ya dijitali wa Benki hiyo hapa nchini.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 


















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































