#Football #Sports

JUDE APEWA KADI NYEKUNDU

Jude Bellingham aliiongoza Real Madrid katika mechi ya mchujo ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Manchester City, lakini wiki yake ikabadilika haraka.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza alitolewa kwa kadi nyekundu katika kipindi cha kwanza huku Los Blancos wakiangusha pointi mbili katika mbio za kuwania taji la Uhispania Jumamosi uwanjani Osasuna.

Kiungo huyo angalau atakuwa safi kwa mechi ya mkondo wa pili dhidi ya City kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu siku ya Jumatano, huku Madrid wakiwa mbele kwa mabao 3-2 baada ya ushindi wao kwenye Uwanja wa Etihad wiki iliyopita.

Ilikuwa ni kadi yake ya pili nyekundu kwa kuzozana na waamuzi tangu awasili Uhispania akitokea Borussia Dortmund mwaka 2023.

Imetayarishwa na Nelson Andati

JUDE APEWA KADI NYEKUNDU

NZOIA SUGAR WAZIDI KUTATIZIKA

JUDE APEWA KADI NYEKUNDU

SIASA MBAYA HATARI KWA MAENDELEO, KINDIKI

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *