#Local News

KRA YAKANA MADAI YA KUONGEZA USHURU

Mamlaka ya Ukusanyaji Ushuru nchini, KRA, imesema haijaongeza ushuru wa biashara, bali inatekeleza tu viwango vya ushuru vilivyoidhinishwa na Bunge.

Kamishna wa Forodha wa KRA, Lilian Nyawanda, amesema hayo akijibu malalamiko ya wafanyabiashara hapa jijini Nairobi. Wafanyabiashara wamekuwa wakilalamikia ongezeko la gharama za kufanya biashara.

Nyawanda amesema KRA haina mamlaka ya kuongeza ushuru bila idhini ya Bunge, na kwamba inatekeleza sheria na viwango vya ushuru vilivyopitishwa na wabunge.

Imetayarishwa na Jesca Angeyo

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *