#Local News

MUSALIA MUDAVADI KUMWAKILISHA RAIS RUTO LUANDA ANGOLA

Waziri Mkuu wa Serikali na Waziri wa Mambo ya Nje Musalia Mudavadi anatarajiwa kuelekea Luanda nchini Angola, ambako atamwakilisha Rais William Ruto katika mkutano wa Umoja wa Afrika, AU, utakaofanyika Agosti 30 mwaka huu.

Mkutano huo utajadili namna ya kuzuia na kumaliza migogoro inayotokea katika nchi mbalimbali za Afrika.

Safari ya Mudavadi inakuja wakati Kenya ikiendelea kushiriki katika juhudi za Umoja wa Afrika za kutafuta amani na kusaidia nchi za Afrika kutatua migogoro kwa njia ya mazungumzo.

Imetayarishwa na Jesca Angeyo

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *