KENYA AIRWAYS YAPOTEZA SHILINGI MILIONI 905 KWA MGOMO
Shirika la Ndege la Kenya Airways limesema limepoteza zaidi ya dola milioni saba, sawa na zaidi ya shilingi milioni 904 kutokana na mgomo wa siku tatu uliovuruga shughuli za usafiri wa anga.
KQ imesema hasara hiyo inajumuisha mapato yaliyopotea pamoja na gharama za malazi, chakula, usafiri na kuwahamisha abiria kwenye safari nyingine.
Wakati wa mgomo huo, ndege 63 zilifutwa na zaidi ya safari 160 kuchelewa kwa wastani wa zaidi ya saa sita, huku zaidi ya tani 370 za mazao na nyama zikishindwa kusafirishwa.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































