#Local News

ASKARI MKUU WA MAGEREZA APATIKANA AMEFARIKI RUIRU

Afisa mkuu wa Huduma ya Magereza amepatikana amefariki ndani ya gari katika eneo Spur Mall, Ruiru, Kaunti ya Kiambu, huku polisi wakianzisha uchunguzi kuhusu kifo chake cha ghafla
Marehemu ametambuliwa kuwa Eric Kiarie Wainaina mwenye umri wa miaka 40, alikua akihudumu katika Makao Makuu ya Kanda ya Kati mjini Nyeri
Polisi wa Kituo cha Mugutha wamesema mwananchi alitoa taarifa baada ya kumwona afisa huyo ndani ya gari aina ya Nissan Wingroad, kabla ya maafisa kufika eneo hilo na kuthibitisha kisa hicho.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *