#Local News

MASENETA WAWAKOSOA MAGAVANA KWA MGOMO WA WAUGUZI

Maseneta wamekosoa Baraza la Magavana kwa kuchelewesha kutatua mzozo wa wauguzi ambao umeathiri huduma muhimu za afya katika hospitali nchini kwa zaidi ya siku 40.

Wakizungumza Seneti baada ya kurejea kutoka mapumzikoni, maseneta wamesema serikali za kaunti zilipewa fedha za kutosha kushughulikia maslahi ya wahudumu wa afya, wakisema kutotatua mgomo huo kunaweza kuzidisha hali ya sekta hiyo.

Wabunge hao pia wametaka kuangaliwa upya kwa wazo la kuanzishwa kwa Tume ya Afya, huku madaktari wakitishia kujiunga na mgomo huo ndani ya siku saba iwapo mzozo hautatatuliwa.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *