CHAMA CHA WAHARIRI CHAITAKA SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATEKAJI WA ALEX KIPROTICH
Chama cha Wahariri nchini kimeitaka serikali kuwatafuta na kuwachukulia hatua waliohusika na kutekwa nyara kwa Mhariri Msaidizi wa kampuni ya Standard Group Alex Kiprotich.
Chama hicho kimesema tukio hilo ni tishio kwa uhuru wa vyombo vya habari na haki ya wananchi kupata habari.
Rais wa Chama hicho Zubeidah Kananu amesema serikali inapaswa kuchukua hatua madhubuti kulinda waandishi wa habari na uhuru wa vyombo vya habari.
Imetayarishwa na Jesca Angeyo
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































